Saturday, September 29, 2012

ZILIPENDWA/JUMAMOSI NJEMA KWA WOTE

Blog ya Maisha na Mafanikio inapenda kuwatakia wote jumamosi njema. Pia nachukua nafasi hii kumshukuru Mungu kwa kunilinda na kujalia afya njema. Pia kwa kuwalinda watu wote na kuwajalia afya njema na kuwapa watu nyoyo zenye huruma na mapendo.JUMAMOSI NJEMA NDUGU ZANGUNI!"!!

Friday, September 28, 2012

Being a Mother/KUWA MAMA

CHUKUA MUDA WAKO /DAKIKA CHACHE NA SOMA HII HABARI AMBAYO NAMI NIMETUMIWA NA MSOMAJI WA MAISHA NA MAFANIKIO BINAFSI IMENIGUSA SANA MPAKA NIMETOA CHOZI..KARIBU.......

After 17 years of marriage, my wife wanted me totake another woman out to dinner and a movie. She said, 'I love you, but I know this other woman loves you and would love to spend some time with you.'
The other woman that my wife wanted me to visitwas my MOTHER, who has been alone for 20 years, but the demands of my work and my two boys had made it possible to visit her only occasionally. That night I called to invite her to go out for dinner and a movie. 'What's wrong, aren't you well,' she asked? My mother is the type of woman who suspects that a late night call or a surprise invitation is a sign of bad news. 'I thought it would be pleasant to spend some time with you,' I responded. 'Just the two of us.' She thought about it for a moment, and then said, 'I would like that very much.' That Friday after work, as I drove over to pick her up I was a bit nervous. When I arrived at her house, I noticed that she, too, seemed to be nervous about our date. She waited in the door. She had curled her hair and was wearing the dress that she had worn to celebrate her last birthday on November 19th. She smiled from a face that was as radiant as an angel's. 'I told my friends that I was going to go out with my son, and they were impressed,' she said, as she got into that new white van. 'They can't wait to hear about our date'. We went to a restaurant that, although not elegant, was very nice and cozy. My mother took my arm as if she were the First Lady. After we sat down, I had to read the menu. Her eyes could only read large print. Half way through the entries, I lifted my eyes and saw Mom sitting there staring at me. A nostalgic smile was on her lips. 'It was I who used to have to read the menu when you were small,' she said. 'Then it's time that you relax and let me return the favor,' I responded. During the dinner, we had an agreeableconversation- -nothing extraordinary but catching up on recent events of each other's life. We talked so much that we missed the movie. As we arrived at her house later, she said, 'I'll go out with you again, but only if you let me invite you.' I agreed. 'How was your dinner date ?' asked my wife when I got home. 'Very nice. Much more so than I could have imagined,' I answered.
A few days later, my mother died of a massive heart attack. It happened so suddenly that I didn't have a chance to do anything for her. Some time later, I received an envelope with a copy of a restaurant receipt from the same place mother and I had dined. An attached note said: 'I paid this bill in advance. I wasn't sure that I could be there; but nevertheless, I paid for two plates - one for you and the other for your wife.You will never know what that night meant for me.I love you, son.'
At that moment, I understood the importance of saying in time: 'I LOVE YOU' and to give our loved
ones the time that they deserve. Nothing in life is more important than your family. Give them the time
they deserve, because these things cannot be put off till 'some other time.'
Somebody said it takes about six weeks to get back to normal after you've had a baby..... somebody
doesn't know that once you're a mother, 'normal' is history. Somebody said you learn how to be a mother by instinct ... . Somebody said being a mother is boring ....somebody never rode in a car driven by a teenager with a driver's permit.
Somebody said if you're a'good' mother, your child will 'turn out good'....somebody thinks a child comes with
directions and a guarantee.Somebody said you don't need an education to be amother.... somebody never helped a fourth grader with his math.
Somebody said you can't love the second child as much as you love the first ..... somebody doesn't
have two children. Somebody said the hardest part of being a mother is labor and delivery....
somebody never watched her 'baby' get on the bus for the first day of kindergarten ...
or on a plane headed for military 'boot camp.' Somebody said a mother can stop worrying after her
child gets married....somebody doesn't know that marriage adds a new son or daughter-in-law to a
mother's heartstrings. Somebody said a mother's job is done when
her last child leaves home..... · somebody never had grandchildren. Somebody said your mother knows you love her, so you don't need to tell her.... Somebody isn't a mother.
This isn't just about being a mother; it's about appreciating the people in your life while you have them....no
matter who that person is.

NAWATAKIENI WOTE MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA HILI..IJUMAA NJEMA !!


NAPENDA KUWATAKIENI WOTE MWANZO MWEMA WA MWISHO WA JUMA!!!

Thursday, September 27, 2012

JINSI YA KUPEANA HABARI KATIKA NDOA ZETU!!!

Tunayo methali isemayo:- "Kisima kikinyauka ndipo tu tunapojua thamani ya maji". Ndivyo ilivyo mara nyingi. Wakati kitu fulani kinapokosekana ndipo tunajua umuhimu wake. Tunapokuwa na afya njema, hatumshukuru Mungu kwa kutujalia afya nzuri na mwili wenye nguvu. Tukipatwa na maradhi ndiyo tunatambua kuwa afya njema ni kitu chenye thamani kubwa. Hali kadhalika, tunashindwa kuwashukuru rafiki zetu kwa ajili ya wema wao kwetu, lakini tukijikuta katika hali ya upweke na huzuni, ndipo twatambua jinsi urafiki ulivyo na thamani sana kwetu.
Ndivyo ilivyo kuhusu kupeana habari. Mara nyingi natambua uhuhimu wa kuongea na mwenzangu wakati ambapo tunakuwa tunakosa kuongea pamoja kwa muda fulani. Ndipo tunatambua kile kinachokosekana, tunaona kila kinachotutenganisha. Hapa tunajaribu kuona jinsi hali inavyokuwa wakati ambapo huna uhusiano mwema katika kupeana habari, na pia mambo gani ya kuhuzunisha hutokea wakati uhusiano unapokuwa si mzuri katika kupeana habari au kutopeana habari kabisa kati ya watu wawili.

Ebu tuangalie mfano huu:- John na maria waliishi katika ndoa kwa muda wa miaka miwili. Walipendana lakinai hakuna aliyemwambia mwenzake juu ya jambo hili. Waliamini ya kwamba kwa kawaida watu wawili waliooana wanapendana, sivyo? Lakini Maria alikuwa na mashaka na Joha. Wakati walikwenda kwenye sherehe au sikukuu fulani, John aliwasifu rafiki zake Maria jinsi walivyokwatua na kuvaa malidadi na jinsi walivyosuka nywele zao. Hata mara moja hakumsifia mkewe au kusema neno lolote la namna hiyo. Maria hakuthubutu kumwambia John juu ya jambo hili. Alizidi kukaa kimya. Siku moja, John alimwuliza Maria, Una nini Maria? Unaonekana huna furaha wakati wote, Hakuna kitu chochote, bali nimechoka tu siku hizi, alijibu Maria.
Kumbe, Maria alikuwa anasema uwongo. Alijua kwamba alikuwa hasemi Ukweli. Lakini John hakujua. Baada ya miezi mitatu kulizuka ugomvi kati ya John na Maria kuhusu fedha, na ndipo ukweli ukaonekana. Kwa kweli Maria hakugombana kwa ajili ya fedha hata kidogo ilikuwa tu ni kisingizio kilichotafutwa ili kuanzisha maneno makali. Sababu ya kweli ilikuwa kwamba Maria alihisi kwamba John alikuwa hampendi tena bali mapendo yake yalielekea kwa wanawake wengine. Kitu kidogo; yaani, kuacha kumsifia na kumwonea fahari mkewe ampendaye kweli, sasa kimekuwa kitu kikubwa, yaani Maria amekuwa na mashaka juu ya mapendo ya mumewe kwake. Kupeana habari kati yao kumekosekana na kitendo hiki kikikomaa, mambo madogo hugeuka kuwa makubwa.
chanzo: KITABU CHA NJIA YETU KWA MAPENDO NA NDOA.
--------------------------------------------------------------------------------------------------------
Ujumbe wangu ni kwamba katika ndoa tuwa na MAWASILIANO NI MUHIMU SANA.

Wednesday, September 26, 2012

UWANJA WA MPIRA MAJIMAJI SONGEA KWA NJE UPANDE WA KULIA KARIBU NA JENGO LA POLISI...!!!

Nimeona tutembelee Songea mjini leo kwani siku nyingi  zimepita. Kila la kheri....

WAREMBO WA WIKI:- HIVI HAPA NI SARESARE AU??!!!


Jinsi bendera ya Tanzania inavyoveza kutukuzwa. Nimependa hii
Na hapa pia ..nimelipenda gauni hili kwanza ndefu, mtindo mzuri na linavutia. Swali wapi nitalipata kwani nimevutiwa sana nayo...

Tuesday, September 25, 2012

MAISHA:- EBU CHUKUA MUDA NA USOME HABARI HII....MAISHA YA NDOA /TALAKA AU ???

Habari hii nimetumiwa na msomaji wa Maisha na Mafanikio . Nikachukua muda na kusoma kwa kweli lazima niseme habari hii imenisikitisha pia nimejifunza jambo nasikutaka kuwa mchoyo kwa vile aliyenitumia hajawa mchoyo kwangu tunagawana elimu huu ndio msingi. Na ndio nimeona niweke hapa kibarazani ili wengi tujifunze maisha yalilivyo. KARIBUNI MUUNGANE NAMI.
--------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------------
“Nilipofika nyumbani usiku ule, mke wangu aliponitayarishia chakula, nilimshika mkono na kumwambia, Kuna kitu nataka nikwambie. Mke wangu alikaa chini na kula chakula kimya akiwa tayari kunisikiliza. Tena nikagundua macho yake yalionyesha anaumizwa. Nilishindwa hata namna ya kuanza kufumbua kinywa changu. Lakini ilibidi nimwambie ili ajue nilikuwa nikifikiri nini juu yake.
Nataka kukupa talaka. Nilianza kusema kwa utulivu. Alionekana kutokereka na maneno yangu badala yake aliniuliza kwa sauti ya upole ‘kwa nini?’ Sikumjibu swali lake. Kutojibu kulimfanya akasirike. Akatupa kijiko na akanikaripia, ‘wewe si mwanamume!’ Usiku ule, hakukuwa na maongezi kati yetu. Alikuwa akilia kwa kwikwi. Nilifahamu kwamba alitaka kujua ni nini kimetokea kwenye ndoa yetu. Lakini kwa hakika nisingeweza kumpa jibu wala sababu ya kuridhisha; alionekana si mali kitu kwangu penzi langu lilihamia kwa Jane. Sikumpenda tena mke wangu mawazo yote yalikuwa kwa Jane. Kwa kweli nilimdharau mke wangu!
Huku moyo wangu ukijua wazi kwamba nafanya kosa, niliandika talaka ambayo ilionyesha kwamba yeye (mke wangu) angepata nyumba yetu, gari na atakuwa na hisa 30% ya kampuni yetu. Aliangalia talaka ile na kuichana vipande vipande.
Mke ambaye tumeishi nami kwa miaka 10 alionekana mgeni machoni mwangu. Nilimuonea huruma kwa muda, rasilimali na nguvu alizopoteza lakini sikuweza kurudi nyuma kwa sababu Jane aliuteka moyo wangu kisawasawa. Hatimaye mke wangu alilia kwa sauti mbele yangu, jambo ambalo kwa hakika nilitarajia. Kwangu mimi kilio chake kilinipa nafuu.
Wazo la kuachana na mke wangu limenisumbua kwa majuma kadhaa na sasa limeendelea kuimarika na kuwa jambo la hakika zaidi.
Siku iliyofuata nilikuja nyumbani kwa kuchelewa sana nikakuta mke wangu akiandika jambo mezani. Sikutamani hata kula chakula alichonipikia nilikwenda moja kwa moja chumbani na usingizi ulinichukua mara moja kwa sababu nilikuwa nimechoka baada ya kula raha za kufa mtu na Jane.
Usiku nilishtuka usingizini mke wangu alikuwa bado akiandika. Sikujali kabisa nikajifunika vyema shuka na kulala tena. Asubuhi yake alinikabidhi masharti ya talaka yake: hakutaka kitu chochote kutoka kwangu lakini alihitaji apate angalau mwezi mmoja wa kujiandaa kabla hajaachika. Akaomba kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja sote mimi na yeye tujitahidi kuishi maisha ya upendo au kawaida kwa kadiri itakavyowezekana. Sababu yake ilikuwa ndogo lakini muhimu: mwanetu wa kiume alikuwa akikaribia kufanya mtihani katika mwezi uliofuata kwa hiyo hakupenda mtoto aathirike kisaikolojia kwa sababu ya kuachana kwetu. Hili halikuwa tatizo kwangu, nilikubali mpango wake. Lakini alikuwa na sharti la ziada, aliniomba nikumbuke jinsi nilivyombeba siku za fungate yetu hasa siku ya harusi yetu. Akaniomba na kunisihi kwamba katika kipindi hicho cha mwezi mmoja niwe nambeba kutoka kitandani kwetu mpaka mlango wa kutokea kila asubuhi. Nilidhani anakaribia kuwa kichaa. Ili kufanya siku zetu za mwisho zisiwe na migogoro nilikubaliana na masharti yake ya ajabu.
Nilimsimulia Jane kuhusu masharti ya kuachana na mke wangu. Jane alicheka sana, aliona ni ujinga. ‘Hata akitumia ujanja wa namna gani talaka ni lazima’, alisema Jane tena kwa dharau. Mimi na mke wangu hatukuwahi kugusana tangu nilipomweleza dhamira ya kumtaliki. Kwa hiyo nilipombeba kwa mara ya kwanza sote tulinuniana. Mwanetu alifurahi sana na kupiga makofi nyuma yetu, ‘aah baba kambeba mama mikononi mwake’. Maneno yake yalinichoma moyoni moja kwa moja. Kutoka chumbani kwetu hadi sebuleni, halafu tena mpaka mlangoni, ni zaidi ya mita kumi nimembeba mke wangu. Alifumba macho na kusema kwa sauti laini na ya upole; usimwambie mwanetu juu ya talaka. Nilikubali kwa kichwa, ingawa nilijisikia vibaya. Nilimuweka chini nje ya nyumba.
Alienda kituoni kusubiri basi la kazini kwake nami nikaendesha gari kwenda ofisini kwangu. Siku ya pili, zoezi lilikuwa rahisi kwetu sote. Aliegemea kifuani pangu. Nilisikia harufu nzuri ya uturi aliofukiza kwenye blauzi yake. Nikagundua kwamba sijamuangalia kwa makini mke wangu kwa kipindi kirefu sana. Nikagundua hakuwa binti tena. Kulikuwa na mikunjo usoni na nywele zake zilianza kuwa nyeupe! Ndoa yetu imekula urembo wake. Kwa dakika moja nikafikiri kwa nini namfanyia hivi.
Siku ya nne nilipombeba hisia za mapenzi kati yetu zilirejea. Huyu ni mwanamke aliyejitoa kuishi nami na tumeishi kwa miaka kumi sasa. Siku ya tano na ya sita ilikuwa wazi kwamba mapenzi yetu yalikuwa yakimea upya. Sikumwambia Jane kuhusu jambo hili. Kadiri mwezi ulivyokaribia kwisha niliona raha kumbeba mke wangu na zoezi likawa rahisi zaidi. Pengine kufanya kazi hii kila siku kuliniimarisha zaidi.
Alikuwa akichagua nini cha kuvaa asubuhi. Alichagua mavazi kadhaa hakupata linalomfaa. Kisha akaguna, ‘nguo zangu zote zimekuwa kubwa’. Nikagundua kwamba mke wangu amepungua sana, nadhani ndiyo maana niliweza kumbeba kirahisi. Ghafla jambo likanichoma... mke wangu ana uchungu na maumivu makuu moyoni mwake. Bila kujitambua nikamgusa kichwa chake. Mara mtoto wetu akatokeza na kusema ‘baba ni wakati wa kumbeba mama muende kazini’. Kwake kumuona baba akimbeba mama likawa ni jambo la furaha sana. Mke wangu alimuonyesha ishara mwanetu asogee karibu na akamkumbatia kwa upendo mkuu. Niligeuza uso wangu nisije nikabadili mawazo katika dakika ya mwisho. Kisha nikambeba mikononi mwangu kutoka chumbani, sebuleni halafu mpaka mlangoni. Mkono wake laini ulikuwa umeizunguka shingo yangu kwa upendo. Nilimkumbatia mwili wake; ilikuwa ni mithili ya siku ya ndoa yetu. Lakini wepesi wake ulinitia mashaka.
Siku ya mwisho nilipombeba nilipata shida hata kupiga hatua moja. Mtoto wetu alishakwenda shuleni. Nilimshika kwa karibu na kumwambia sikubaini kwamba maisha yetu yalikosa upendo. Nikaenda zangu ofisini…. Nikashuka garini hata bila kufunga mlango. Maana nilihisi nikichelewa tu ninaweza kubadili nilichoamua.... nikapand ngazi. Jane alifungua mlango nikamwambia, ‘Samahani, Jane, sihitaji tena kumtaliki mke wangu’. Akaniangalia kwa kustaajabu, halafu akagusa kichwa changu. Akaniuliza ‘Unaumwa?’ Nikaondoa mkono wake kichwani kwangu. ‘Samahani, Jane, nimesema sitaki kumtaliki mke wangu. Nadhani ndoa yangu haikuwa na furaha kwa sababu sikuthamini undani wa maisha yetu, mimi na mke wangu, si kwamba hatupendani. Nimetambua hilo tangu nilipombeba siku ya ndoa yetu nilitakiwa kumbeba siku zote za maisha yetu, nampenda mke wangu sitamuacha mpaka kifo kitakapotutenganisha.’
Ikawa kama Jane alizinduka usingizini. Akanizaba kibao cha nguvu, akajiegemeza mlangoni na kuanza kulia. Nikashuka ngazi na kuondoka zangu. Nikaingia kwenye duka la maua nikaagiza maua mengi mazuri kwa ajili ya mke wangu. Muuzaji akaniuliza aandike nini kwenye kadi. Nikatabasamu na kuandika “Nitakubeba kila asubuhi mke wangu mpaka kifo kitakapotutenganisha”. Jioni ile nilifika nyumbani na maua mikononi mwangu, tabasamu kubwa usoni nikakimbia mpaka chumbani, nikapokelewa na maiti ya mke wangu kitandani.
Kumbe mke wangu alikuwa akisumbuliwa na saratani kwa miezi kadhaa nami nilishindwa kubaini kwa sababu nilihamishia akili yangu kwa Jane. Alijua kwamba angekufa karibuni na alitaka asiniingize katika chuki na mwanetu kama ningelazimisha talaka mapema.
Angalau machoni mwa mwanangu naonekana ni mume mwema….
Jamani vitu vidogo vidogo vizuri ni vya msingi sana katika mahusiano yetu... Siyo majumba au magari au fedha zilizoko kwenye benki. Hivi vitakupa tu mazingira ya kufurahi lakini vyenyewe siyo furaha. Kwa hiyo jitahidi kuwa na muda mzuri na mazingira rafiki ya kuwa na mwenzi wako, kuwa rafiki wa mwenzi wako. Fanya vitu mlivyofanya wakati wa uchumba na wa ndoa yenue ambavyo vitawaweka karibu siku zote. Muwe na ndoa yenye furaha. Mara nyingi watu hushindwa katika ndoa kwa kutotambua ni kwa kiasi gani walikuwa karibu wakati wa kujenga uhusiano wao
Mungu awabariki nyote mliosoma na kujifunza hapa.

SINA WASIWASI NIPO SAFARINI NIKIWA NA MLINZI WANGU...!!!

Nimeipenda picha hii imenikumbusha Mgazini, huu udongo jinsi ulivyo mwekundu hapo kuvaa nguo nyeupe inabidi uwe msafi sana. Wanafunzi walikuwa/wanapata shida sana maana ukivaa shati jeupe siku moja tu  ni lazima kufua. Halafu nimeipenda hii picha jinsi mama huyo anavyosafiri huku mbwa wake katangulia kama mlinzi. Mlinzi wa asili.

Monday, September 24, 2012

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA JUMAPILI YANGU YA 24/92012:- ILIKUWA JUMAPILI NJEMA SANA ....

Jumapili ya jana ilikuwa sio kama jumapili nyingine. Jumapili hii kulikuwa na ugeni kutoka Tanzania Huyo  baba mwenye suti nyeusi ni baba askofu na anatokea njombe ila anafanya kazi Dodoma na mwenye nguo za kijiani kijana ni mke wake halafu walikuwa wakaka watatu ambao ni wamasai...Kama kawaida Kapulya hakukosa kuuliza maswali hapa nilijikuta nipo nyumbani kabisa kuonana na waTanzania wenzangu na kuongea kiswahili kwa raha zote pia kibene. Majina yao nimesahau kidogo...

Hapa hadithi zimekolea na wote tupo ndani ya kicheko  kama muonavyo....

 Ndani ya kanisa

Friday, September 21, 2012

BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO INAPENDA KUWATAKIENI MWANZO NA MWISHO WA JUMA HILI UWE MWEMA...HAKI IKO WAPI NA SUSUMILA FT MAHATMA


JIJUMAA NJEMA KWA WOTE!!!

TANGAZO:-NUFAIKA NA KILIMO ANZA SASA!!!

WEWE NI MKULIMA STADI? …… HUJACHELEWA ……. ANZA SASA ….
Fesh Farms (T) sasa wanasaidia uwekezaji katika kilimo cha miti ya
nguzo, karatasi na mbao. Wanauza mashamba yenye miti (ardhi pamoja na
miti); maeneo ya Mufindi-Iringa (kilomita 75 kutoka Iringa mjini). Bei
ni tsh 600,000 hadi 1,000,000 kwa ekari. Umri wa miti ni miaka 1 hadi
5. Unaweza kununua ekari kuanzia moja na kuendelea. Fresh Farms (T)
wana magari yatakayokupeleka na kukurudisha mashambani ikiwa unataka
kuyaona, kujifunza ama kununua.
Pia tunauza mashamba tupu (ardhi tupu) kwa 100,000 hadi 200,000 tu kwa
ekMashamba yote yana "documents" za umiliki na Fresh Farms (T)
itaendelea kukusaidia kutunza mashamba uliyonunua, hadi kuvuna miti
kwa gharama na utaratibu nafuu kabisa.
NB: Muda wa kuvuna miti ya mbao tangu kupandwa ni kuanzia miaka sita,
miti ya nguzo inavunwa baada ya miaka 4-5 tangu kupandwa. Miti
iliyokomaa kwa ekari moja unaweza kuvuna mbao hadi za shilingi 12M.
Wasiliana nasi kwa anuani zifuatazo
Fresh Farms (T)-Albert Sanga (Director) 0766 742414/0719 127 901
e-mail; stepwiseexpert@googlemail.com
Markus Mpangala (Advertising Officer)- 0764936655
e-mail: mwanazuoni27@gmail.com

Thursday, September 20, 2012

KISA CHA KWELI !!!!


Nimetumiwa kisa hiki na msomaji wa Maisha na Mafanikio. Nikachukua muda na kusoma kwa kweli lazima niseme kisa hiki kimenigusa sana na nikaona kwamba msomaji huyu hajawa mchoyo kwangu kwanini mimi niwe mchoyo nimeona niweke hapa kibarazani ili wengi tujifunze maisha yalilivyo. KARIBUNI MUUNGANE NAMI.
................................................................................................................................................................
Ni siku nyingi kidogo, mwaka 1979, lakini ni tukio ambalo liliniuma sana. Ilikuwa vigumu sana kulisahau na lilinifanya nijiulize, inakuwaje Mungu anakuwa mkatili kiasi kile. Lakini bila shaka ilikuwa ni wakati ule wa ufahamu mdogo. Hivi sasa ninafahamu mengi na hasa baada ya kujifunza maarifa haya ya utambuzi.

Ilikuwa ni mwaka 1979 nikiwa nasafiri kutokea Dar es salaam kwenda Arusha. Sijui ilikuwaje, lakini ilitokea. Tuliondoka Dar es salaam saa 12.30 jioni. Wakati ule mabasi yalikuwa yakisafiri jioni na usiku, sio kama siku hizi.

Nilikuwa ninakwenda Arusha kwenye usaili kwa ajili ya ajira, nikiwa ndio kwanza nimemaliza kidato cha nne. Niliajiriwa moja kwa moja serikalini, kwani siku zile ajira zilikuwa ni za kumwaga. Hata hivyo sikuridhishwa na kazi niliyokuwa nafanya, hivyo niliomba kazi kwenye kampuni moja kule Arusha na niliitwa kwa usaili.

Tulifika mji unaoitwa Korogwe ambao wakati ule ulikuwa ndio mji maarufu kwa hoteli zake katika barabara yote ya Segera hadi Moshi na Arusha. Tulipofika Korogwe basi letu lilisimama kwa ajili ya abiria kupata chakula. Niliingia kwenye hoteli moja ambayo nakumbuka hadi leo kwamba ilikuwa ikiitwa Bamboo. Niliagiza chakula na kula haraka kutokana na muda mfupi wa kula uliotolewa na wenye basi la TTBS ambalo ndilo nililosafiri nalo.

Wakati wa kulipa ndipo niliposhangaa na kuogopa. Niliingiza mkono mifukoni na kukuta kwamba sikuwa na hela. Nilianza kubabaika na mwenye hoteli alisema hawezi kukubali ujinga huo, "Abiria wengine wahuni bwana, anakula na kujifanya kaibiwa, ukikubaliana nao kila siku hasara tu" Mwenye hoteli alisema kwa kudhamiria hasa.

Kulizuka zogo kubwa, huku mwenye hoteli akisema ni lazima anipeleke polisi. Ni kweli alimtuma mmoja wa watumishi wake kwenda kituo cha polisi ili nishughulikiwe……

Hapo Hotelini kulikuwa na bwana mmoja aliyekuwa amekaa pembeni na mkewe na watoto wao wakila. Yule bwana alipoona vile alimtuma mhudumu mmoja aniite. Niliondoka pale kaunta nilipokuwa nabembeleza na kuja kwa yule bwana.

Alikuwa ni kijana mtu mzima kidogo, mwenye miaka kama 50 hivi. Nilimsalimia na aliitikia, nilimsalimia mkewe pia. Yule bwana aliniuliza kisa cha vurugu ile na nilimsimulia. Aliniuliza sasa huko Arusha ningeishi vipi wakati wa usaili wakati nimeibiwa fedha zote na ningerudi vipi Dar. Nilimwambia nilikuwa napanga namna ya kurudi Dar, kama huko polisi ningeaminika.

Kama mzaha vile yule bwana aliniambia kuwa angenipa fedha za kutumia huko Arusha na nikirudi Dar nimrudishie fedha zake. Nakumbuka alinipa shilingi 90 kwa ahadi kwamba nikirudi Dar nimpelekee fedha zake ofisini kwake. Alinielekeza ofisini kwake, mtaa wa Nkuruma na kuniambia kuwa ameamua kunisaidia kwa sababu kila binadamu anahitaji msaada wa mwingine na maisha haya ni mzunguko. Nilimshukuru na kuondoka kukimbilia basini. Basi lilikuwa linanisubiri mimi tu. Nilipanda ndani ya basi na abiria wengine walinipa pole. Tuliondoka Korogwe, lakini haikuchukua muda basi letu lilipata tatizo la pancha ya gurudumu moja la mbele. Ilibidi tuegeshe pembeni ili litengenezwe. Baada ya matengenezo, tuliondoka kuendelea na safari yetu.

Karibu na mji wa Same kwenye saa saba usiku, basi letu lilisimama ghafla. Abiria walisimama ndani ya basi na kulizuka aina ya kusukumana. Huko nje kulikuwa na ajali. Abiria tulishuka haraka na wengine huko chini walishaanza kupiga mayowe, hasa wanawake. Niliposhuka niliona gari ndogo nyeusi ikiwa imebondeka sana na hapo kando kulikuwa na maiti wawili.

Nilijua ni maiti kwa sababu walikuwa wamefunikwa gubigubi. Halafu kulikuwa na katoto kalikokuwa kanalia sana kakiwa kamefungwa kanga kichwani. Tumwahishe huyu mtoto hapo Same hospitali ameumia, ingawa sio sana. Nilikatazama kale katoto ka kiume kenye umri wa miaka kama mitatu. Kalikuwa kameumie kwenye paji la uso, lakini kalikuwa hai. Bila shaka wale walikuwa ni wazazi wake, kalikuwa yatima tayari. Machozi yalinitoka.

Baada ya kupata msaada na askari wa usalama barabarani kuchukua maiti wale tulipanda basini kuendelea na safari yetu. Kale katoto kalichukuliwa na jamaa fulani waliokuwa na Land Rover ya serikali kukimbizwa hospitalini. Ndani ya Basi mazungumzo yalikuwa ni kuhusu ajali ile tu, hadi tunafika Arusha. Tulichelewa sana kufika Arusha kwani tulifika kwenye saa tano asubuhi, badala ya saa mbili .

Nililala kwenye hoteli rahisi na kufanya usaili kesho yake. Ni hiyo kesho, baada ya usaili niliponunua gazeti ambapo nilipata mshtuko mkubwa ajabu. Kumbe wale watu wawili waliokufa kwenye ajali ile ya Same walikuwa ni yule bwana aliyenisaidia hela na mkewe. Yule mtoto wao ndiye aliyeokoka. Niligundua hilo baada ya kusoma jina lake na jina la kampuni aliponiambia nimpelekee fedha zake nikirudi Dar, pamoja na picha yake, mke na mtoto. Nililia sana, kama mtoto.

Nillishindwa kujua ni kwa nini afe. Nilijiuliza ni nani sasa angemlea mtoto yule? Yalikuwa ni maswali yasiyo na majibu na pengine maswali ya kijinga pia.
Nilijua kwamba nilikuwa na deni, deni la shilingi tisini. Kwa wakati ule shilingi tisini zilikuwa ni sawa na shilingi laki moja za sasa.
Kwa mara ya kwanza sasa nilijiuliza ni kwa nini marehemu yule aliniamini nakuamua kunipa fedha zile. Sikupata jibu.

Nilikata kipande kile cha gazeti la kingereza kilichokuwa na habari ile. Nilichukuwa kipande hicho na kukiweka kwenye Diary yangu. Deni, Ningelipa vipi deni la watu? Nilijikuta nikipiga magoti na kuomba mungu anipe uwezo wa kuja kulilipa deni la mtu yule mwema kwa njia yoyote. 'Mungu naomba uje uniwezeshe kulilipa deni la marehemu kwa sura na namna ujuavyo wewe. Nataka kulilipa deni hili ili nami niwe nimemfanyia jambo marehemu,' niliomba. Nilirejea Dar siku hiyo hiyo.Kwa sababu ya mambo mengi na hasa baada ya matokeo ya usaili ule kuwa mbaya kwangu, nilijikuta nikiwa na mambo mengi na kusahau haraka sana kuhusu mtu yule aliyenisaidia mbaye ni marehemu. Nilifanikiwa hata hivyo kupata nafasi ya kusoma Chuo cha Saruji na baadae chuo cha ufundi na hatimaye nilibahatika kwenda nchini Uingereza. Mwaka 1991 nilianza shughuli zangu.

Ilikuwa ni mwaka 1995 nikiwa ofisini kwangu pale lilipokuwa jengo Nasaco ambalo liliungua mwaka 1996, ambapo lilijengwa upya na kubadilishwa jina na kuitwa Water Front. Nikiwa nafanya kazi zangu niliambiwa na sekratari wangu kwamba kulikuwa na kijana aliyekuwa anataka kuniona. Nilimuuliza ni kijana gani, akasema hamjui. Nilimwambia amruhusu aingie. Kijana huyo aliingia ofisini. Alikuwa ni kijana mdogo wa umri miaka kama 17 au 18 hivi, mweupe mrefu kidogo. Alikuwa amevaa bora liende , yaani hovyohovyo huku afya yake ikiwa hairidhishi sana.

Nilimkaribisha ilimradi basi tu, kwani niliona atanipotezea bure muda wangu. Ni lazima niwe mkweli kwamba sikuwa mtu mwenye huruma sana na nilikuwa naamini sana katika watu wenye pesa au majina. Nilimuuliza, “nikusaidie nini kijana na ukifanya haraka nitashukuru maana nina kikao baada ya muda mfupi”. Nilisema na sikuwa na kikao chochote , lakini nilitaka tu aondoke haraka.

“Samahani mzee, nilikuwa na shida…..nimefukuzwa shule na sina tena mtu wakunisaidia kwa sababu …..nime….niko ….kidato cha pili na hivyo tu natafuta tu kama atatokea mtu……..
Nilimkatisha. “Sikiliza kijana. Kama huna jambo lingine la kusema, ni bora ukaniacha nifanye kazi. Hivi unafikiri kama nikiamua kumsaidia kila mtu aliyefukuzwa shule si nitarudi kwetu kwa miguu! Nenda Wizara ya Elimu waambie……Kwanza wazazi wako wanafanya kitu gani, kwa nini washindwe …..Kwa nini walikupeleka shule ya kulipia kama hawana uwezo, wanataka sifa?”

“Hapana wazazi wangu walikufa na ninasoma shule ya serikali. Nimekosa mahitaji ya msingi na nauli ya kwendea shule. Nasoma shule ya Kwiro, Morogoro. Shangazi ndiye anayenisomesha, naye ana kansa na hivi sasa hata kazi hafanyi….,” Alianza kulia. Huruma fulani ilinijia na nilijiambia, kama ni nauli tu na matumizi, kwa nini nisiwe mwema, angalau kwa mara moja tu. “Baba na mama walifariki lini?” Niliuliza nikijua kwamba, watakuwa wamekufa kwa ukimwi, maana kipindi kile ndipo fasheni ya ukimwi ilipoanza, ambapo kila anayekufa huhesabiwa kwamba kafa kwa ukimwi.

“Walikufa kwa ajali nilipokuwa mdogo sana, nilipokuwa na miaka mitatu. Ndio shangazi yangu akanichukua na kunilea hadi sasa anakufa kwa kansa.” Yule kijana alilia zaidi. Naomba nikwambie wewe msomaji unayesoma hapa kwamba, kuna nguvu fulani na sasa naamini kwamba ziko nyingi ambazo huwa zinaongoza maisha yetu bila sisi kujua.

Kitu fulani kilinipiga akilini paaa! Nilijikuta namuuliza yuel kijana. “Kwa nini umeamua kuja kwangu, ni nani alikuelekeza hapa na wazazi wako walikufa mwaka gani na wapi?”
Yule kijana alisema, “Nimeona nijaribu tu kwa mtu yeyote ambaye anaweza kunisaidia, na ndio nimejikuta nikiingia hapa, sijui……..sikutumwa na mtu. Wazazi wangu walikufa mwaka 1979 huko Same na mimi wanasema nilikuwa kwenye ajali, nikaokoka. Niliumia tu hapa.” Alishika kwenye kovu juu ya paji lake la uso.

Nilihisi kitu fulani kikipanda tumboni na kuja kifuani halafi niliona kama vile nimebanwa na kushindwa kupumua. “Baba yako alikuwa anaitwa nani?” “Alikuwa anaitwa Siame….Cosmas Siame….” Niliinuka ghafla hadi yule kijana alishtuka . Nilikwenda kwenye kabati langu mle ofisini na kuchakura kwenye droo moja na kutoka na diary. Mikono ikinitetemeka, nilitoa kipande cha gazeti ndani ya diary hiyo, nilichokuwa nimekihifadhi.

“Ndio alikuwa anaitwa Cosmas Siame. Huyu ni mtoto wake, ni yule mtoto aliyenusurika.” Nilinong’ona. Nilijikuta nikipiga magoti na kusali. “Mungu, wewe ni mweza na hakuna kinachokushinda. Nimeamini baba kwamba kila jema tunalofanya ni akiba yetu ya kesho na kesho hiyo huanzia hapa duniani.” Halafu nillinyamaza na kulia sana. Nililia kwa furaha na ugunduzi wa nguvu zinazomgusa binadamu kwa kila analofanya.

Nilisimama nikiwa nimesawajika kabisa. Nilihisi kuwa mtu mwingine kabisa. Nilimfuata yule kijana na kumkumbatia huku nikiwa bado ninalia. “Mimi ni baba yako mdogo, ndiye nitakyekulea sasa. Ni zamu yangu sasa kukulea hadi mwisho” Naye alilia bila kujua sababu na alikuwa amechanganyikiwa kabisa. Nilirudi kwenye kiti na kumsimulia kilichotokea miaka 17 iliyopita.

Tuliondoka hapo na kwenda kumwona shangazi yake Ubungo, eneo la maziwa ambako alikuwa amepanga chumba. Kutokana na hali yake nilimhamishia kwangu, baada ya kumsimulia kilichotokea. Huyo dada yake Cosmas alifurahi sana hadi akashindwa kuzungumza kwa saa nzima. Alifariki hata hivyo mwaka mmoja baadae, lakini akiwa ameridhika sana.

Kijana Siame alisoma na kumaliza Chuo Kikuu na hivi sasa yuko nchini Australia anakofanya kazi. Ukweli ni kwamba ni mwanangu kabisa sasa. Naamini huko waliko Mbinguni wazazi wake wanafurahia kile walichokipanda miaka mingisana nyuma. Lakini nami najiuliza bado. Ilikuwaje Cosmas akanipa msaada ule? Halafu najiuliza ni kitu gani kilimvuta mwanae Siame hadi ofisini kwangu akizipita ofisi nyingine zote? Nataka nikuambie, usiwe mbishi sana bila sababu, kuna nguvu za ziada zinazoongoza matokeo maishani mwetu…………

*************MWISHO*********

Wednesday, September 19, 2012

SHUKRANI ZANGU...



Chacha wambura Ng´wanambiti
Katika maisha, watu wengi hufikiri watu wa karibu yaani ni familia tu. Leo nimehakikisha kitu ambacho sitaweza kusahau maishani mwangu. Watu/mtu anachukua muda wake na kufanya kitu ambacho wengi hawangefanya. Huyu kaka sijawahi kuonana naye lakini kama alivyosema hapa kwake hakika ni wachache sana wanafanya hivi. Mwenyezi Mungu na akubariki na akuzidishie upendo. Ahsante sana.

Tuesday, September 18, 2012

UJUMBE WANGU WA LEO:- WASICHANA NA WANAWAKE WANA HAKI!!

Watu wote ni sawa, watu wote wana thamani sawa. Hii ina maana kuwa wanawake na wanaume, wasichana na wavulana, wana haki sawa. Lakini katika jamii zetu wanawake na wasichana wananyimwa haki zao.
Hatua ya kwanza kuleta usawa ni kuielewa na kutokuukubali unyanyasaji wa wanawake na wasichana
JUMANNE NJEMA NDUGU ZANGUNI!!!

Monday, September 17, 2012

HIVI NDIVYO ILIVYOKUWA IIJUMAA YANGU/WIKIENDI YANGU PAMOJA NA WAFANYAKAZI WENZANGU!!!

 Kula pilau au kujisikia upo Afrika/Tanzania si lazima uwe Afrika /Tanzania.Ijumaa ya tarehe 14/9/2012 nikaamua kuwaalika wafanyakazi wenzangu kuja nyumbani kwangu. Nao wakaja na mambo yakawa kama muonvyo. Niliwaomba wabadili nguo na wavae kiafrika nao hawakusita. kama muonavyo hapa chini.
 Hapa ni maandalizi ya kuaandaa pilau/chakula yanaanza
 Baadhi ya wageni wamewasili
 Tupo mezani tunalichapa pilau kwa raha zote
 Msosi na hadithi zinaendelea ,......kila kitu kilikuwepo
Mpishi na mwenyeji anaonekana hapa pia ...maana ndiye alikuwa mpiga picha za hapo juu



Na mwisho akatokea mpiga picha na tukapiga picha ya pamoja. Waliokaa chini kwanza Yasinta, anayefuatia ni Marlene, waliosimama nyuma yangu ni Pernilla, anayefuatia mwenye batiki ni Ylva na halafu Elizabeth na mwisho ni Maria. Nilifurahi sana kuwa walikubali kuvaaa nguo zangu angalia utadhani walipima wao:-) Na jioni ikaishia hapa. Hakika kwangu na kwa wo pia tulikuwa na siku nzuri sana naweza nikasema tulikuwa nusu ya Afrika/Tanzania. JUMATATU NJEMA.

Sunday, September 16, 2012

Ngoja leo tusali Sala ya Wazazi wakiwaombea Watoto wao

Tunawaangalia , Ee BwanaHawa uliotujalia.Katika hawa tunajiona sisi wenyewe. Je, kweli tulikuwa hivi sisi
Tulipokuwa watoto? Tulipigana hivi? Tulipaiga kelele hivi? Tulileta furaha namna hii. Na mateso namna hii kwa wazazi wtu? Tunashangaa na kujiuliza....Tunajaribu kukumbuka-----Kukumbuka jinsi ilivyokuwa
Tulipokuwa watoto wadogo bado. Tukiwatazama watu wakubwa.

Wakati mwingine wanatutia wasiwasi, Bwana. Au kwa namna nzuri zaidi, tunajitia wasiwasi sisi wenyewe
Kwani si rahisi kuwa sawa daima. Lakini kuna furaha pia, furaha kubwa wanayotuletea. Nao hutufanya tuone fahari,kwani ni watoto wema.

Tunakushukuru kwa ajili yao Bwana, wao ndiyo zawadi yako bora kwetu,baada yetu sisi wenyewe. Utusaidie tuunganisha mikono yetu na mkono yako Ili, Ee Baba,Wawe kweli Watoto wetu.
Amina.
JUMPILI NJEMA KWA WOTE

Thursday, September 13, 2012

TUMALIZE SIKU HII KWA PICHA HIZI:- SARESARE MAUA ASIYEJUA KUCHAGUA ....!!!

 Sehemu fulani Jamaica
Je unamjua huyu?
Nimezipenda hizi picha na nimeona ziwe picha za wiki hii. Rangi za mavazi ni rangi ambazo nazipendaaaaaaaa sana. Hakika ukijipenda mwenyewe basi na wengine watakupenda!!

Na sasa ngoja tusikiliza kibao hiki ambacho kinawakilisha ujumbe murwaaaaaaaaaaaaaaaaa.




UJUMBE WA LEO:- HUU NDIYO UPENDO!!!

Ufafanuzi mmoja kuhusu upendo ni, ‘uhusiano mchangamfu na wakibinafsi au shauku yenye kina, kupendezwa sana na mtu mwingine.’
Ni sifa ambayo huchochea watu wafanye mambo yanayowanufaisha wengine, nyakati nyingine wakifanya hivyo kwa kujidhabihu sana. Kulingana naufafanuzi wa Biblia, upendo wahusisha akili na moyo.
Akili, au uwezo wa kufikiri, hutimiza fungu fulani kwasababu mtu anayependa hufanya hivyo akitambua kwamba yeye pamoja na wanadamu wengine anaowapenda, wana udhaifu na vilevile sifa zenye kuvutia.

Uwezo wa kufikiri wahusika hata zaidi kwa kuwa kuna wale ambao Mkristo huwapenda—nyakati nyingine, hata ingawa nyutu zao hazimpendezi—kwa kuwa kutokana na kuisoma Biblia anajua kwamba Mungu anataka afanye hivyo.
Hata hivyo, kwa asili upendo hutoka moyoni. Upendo halisi kama uonyeshwavyo katika Biblia hautegemei tu uwezo wa kufikiri. Wahusisha unyofu mwingi na kujitoa kabisa kihisia-moyo.

Ni nadra sana kwa watu ambao ni wenye ubinafsi kudumisha uhusiano wenye upendo wa kweli kwasababu mtu anayependa huwa tayari kutanguliza masilahi ya mwingine.
Maneno ya Yesu “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko kulivyo katika kupokea” ni ya kweli hasa wakati wa kutoa kunapokuwa tendo la upendo.Upendo ni kifungo chenye nguvu. Mara nyingi upendo hutia ndani urafiki, lakini vifungo vya upendo ni vyenye nguvu zaidi ya vifungo vya urafiki.

Uhusiano wa kimahaba kati ya mume na mke wake nyakati nyingine husemwa kuwa upendo; hata hivyo, upendo ambao Biblia hututia moyo tusitawishe hudumu kuliko uvutio wa kimwili.
Mume na mke wanapopendana kwelikweli, huendelea kuwa pamoja hata isipowezekana tena kuwa na uhusiano wa kimwili kwa sababu ya udhaifu unaosababishwa na uzee au kwa sababu mmoja wao hajiwezi.
UPENDO DAIMA!!!

Wednesday, September 12, 2012

MKOA WA RUVUMA KUPATA CHUO KIKUU CHA MTAKATIFU AUGUSTIN, MJINI SONGEA.!!!

Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustin ni mradi wa Kanisa Katoliki Tanzania. Binafsi nashukuru sana kwa uwepo wa chuo hiki kwa hiyo wana-Ruvuma sasa tuchukue/tuitumie nafasi hii muhimu ya ELIMU ipasavyo. Picha  kutoka hapa. Sitakosa nami kutembelea hapa punde nifikapo Songea.
Ngoja tumalizie na maelezo mafupi hapa....
KILA LA KHERI KWA WOTE.....

Tuesday, September 11, 2012

TUSISAHAU VITENDAWILI VYETU/TUWAFUNZE NA WATOTO WETU!!!KITENDAWILI ...TEGA!!

Unganeni nami ili tupata majibu ya VITANDAWILI HIVI HAPA CHINI. KARIBUNI SANA!!
1. Nyumbani mwangu mna shetani ambaye daima anakunywa maji yangu...
2. Mama nieleke.
3. Nenda huko na nikirudi nimshike ngómbe wa mama mkia.
4. kipo lakini hukioni.
5. Nilikuwa nikitembea njiani niliposimama nikasikia mtu akiniita "wifi! wifi!, lakini nilipogeuka sikumwona mtu.
6. Bibi mweupe ametupwa mibani.
7.Mzazi ana miguu bali mzaliwa hana.
8. Wanabgu wote wamevaa vizibao, wasiovaa si wanangu.
9. Ni nini  hutupwa juu ya meza wakati watu wapo ndani?
10. Huku ngó na kule ngó.
JUMANNE NJEMA KWA WOTE!!!

Monday, September 10, 2012

JUMATATU YA LEO TUANZE KIHIVI..AKINA MAMA/TUNATOKA SHAMBANI KUMALIZIA KUVUNA!!

 Picha hii ilikuwa mwaka "1955 mama huyu amebeba bonge la kikapu, na inasemekana ndani ya kikapu kuna ndizi na kama kawaida mgongoni kabeba mwanae. Hapa ni kando ya ziwa nyasa"
Na hapa ni sasa napo ni vivyo hivyo akina mama /dada wakitoka shamba wengine wamebeba vikapu na kitu ndani na wengine kuni na pia baadhi wamebeba watoto mgongoni ..Je hapa si kweli kwamba akina mama ni ngozo ya familia/jamii?

Sunday, September 9, 2012

KANISA NI KANISA...JUMAPILI NJEMA KWA WOTE!!

Kumwomba mungu/kusali si lazima kuwa  na kanisa la kifahali. Tena inawezekana kanisa kama hili ndio maombi yako yatapokelewa zaidi kuliko kwenye makanisa ya kifahami. Kumwomba Mungu ni sehemu yoyote ile na maombi yatapokelewa. Nimelipenda kanisa hili...JUMAPILI IWE YENYE UPENDO NA BARAKA KWA WOTE.

Friday, September 7, 2012

PALE HALI YA HEWA INAPOBADILIKA /UPWEKE UNAINGIA PIA!!!

 Sasa ndio ule wakati baridi inaanza kunyemelea. Kama uonavyo katika picha majani siyo ya kijani tena isipokuwa ni njano njano. Höst "majira baridi ya kuputika majani"na baada ya hapa kutakuwa na baridi zaidi theruji..brrrrriii. Na sasa  kwa watu waliozoea kujichanganya  ni ngumu sana hakuna mtu/jirani anaonekana nje. Kaaazi kwelikweli..NIWATAKIENI MWISHO WA JUMA MWEMA..TUKISHIRIKIANA/UNGANA TUTAFANIKISHA TU.

Thursday, September 6, 2012

WANADAMU NA TABIA ZETU/CHUKI ZETU....KUSENGENYANA/KUSEMANA HADI MAOFISINI...

Jana nilikuwa naangalia kipindi fulani na hapo ndipo nilipokumbuka. Ya kwamba watu wengi wanasema akina mama/wanawake ni watu ambao wanapenda sana kusemana/kusengenyana. Hapana si wanawake tu nimeona mwenyewe kwa macho yangu na kusikia kwa masikio yangu. Yaani mtu anakuwa rafiki yako na unaongea naye, na unacheke naye na unamwamini kabisa lakini kumbe sio unavyofikiri wewe. Na watu wengi wamekuwa wakigombana/gombanishwa kwa kitu ambacho si cha kweli na mwisho kuishia kuwa madui wakubwa. Kwa nini kusema ya wenzio na yako nani atasema.? Na kwa nini kama tuna nguvu  basi tuchukue jembe na kwenda kulima kuliko kutumia muda na kusema wengine? Na kwa nini mpaka kumsema mwingine? Ni afadhali kuchukua jukumu na kumwambia/kumuuliza tu. Kuliko kusengenya sengenya ...
Ngoja mr. Nice amalizie  kwa TABIA GANI .....

UNAPOMSEMA MWENZAKO JIFIKIRIE MWENYEWE KUWA JE? KAMA NINGESEMWA MIMI NINGEJISIKIAJE?

NILIPOFIKA KWENYE KIWANDA/MASHINE YA KUKOBOA MPUNGA NA KUPATA MCHELE AMBAO NI BORA TANZANIA/KYELA!!!

 Mpunga umeanikwa ili ukobolewa na baadaye kuwa mchele. Nilifika hapa "kiwandani na nikapata mfuko mzima wa mchele. Ambao inasemekana ni mchele bora kwa Tanzania yaani hapa Kyela.....

...Hilo jengo ndimo kazi ya kukoboa inamofanyika.Nilisahau kweli kuwauliza haya madawati ni kwa ajili ya nini?..Nilifurahi sana kufika Kyela kwa mara ya kwanza na kuupata mchele bora wa Kyela. Nadhani wengi mnajua hili kuwa mchele wao ni mzuri, unanukia na mtamu sana. Au je kuna mchele unaweza kuushinda huu?

Wednesday, September 5, 2012

VAZI HILI LA KITENGE NIMELIPENDA SANA..MAMA SALMA KIKWETE NA DKT ASHA-ROSE MAIGIRO

Ndugu zangu waTanzania hasa akina dada/akina mama hebu angalieni vazi/mavazi haya. Kwanza ni la heshima, pili wanapendeza yaani hata kuangalia tu kwa macho. Mara nyingi nimekuwa nikijiuliza kwa nini kupoteza pesa nyingi kununu nguo kama mitumba nk. Wakati kuna vitenge vizuri ajabu ambavyo twaweza kushona na kupendaza kama akima mama hao hapo juu. Angalia mishono yao ni rahisi rahisi tu si ya ajabu. Hakika mwenzenu niMEPENDA SANA HII.
---------------------------------------------------------------------------------------------------------
Hapa ni wote mnawafahamu hawa akina mama ila nitasema tena ni:- Mwenyekiti wa taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete akiwa na aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dkt Asha-Rose Migiro baada ya Mama Kikwete kuzindua Mpango wa Kasi ya Uwezeshaji wa Wanawake na Wasichana Agosti 24, 2012 katika ukumbi wa Kilimanjaro Hyatt Regency jijini Dar es salaam.

JUMATANO NJEMA KWA WOTE!!!!




Tuesday, September 4, 2012

Tafakuri Ya Usiku; Je, Uwezo Wetu Wa Kufikiri Umepungua?


Ndugu zangu,

Yanayotokea nchini mwetu yanatutaka sio tu tufikiri, bali, tufikiri kwa bidii. Lakini swali ni hili; Je, uwezo wetu wa kufikiri umepungua?
Yumkini si kwa aliyekuwa na
ujasiri wa kuipiga picha hiyo hapo juu. Alifikiri sana pia. Na si kwa aliyekaa chumba cha habari na kuumiza kichwa, kisha akaamua picha hiyo ipambe sura ya mbele ya gazeti la Mwananchi la juzi. Hapa Iringa gazeti hilo liligombaniwa kama njugu, na bila shaka sehemu nyingine za nchi.
Naam, siku hizi utasikia ikisemwa; " Tumefika pabaya!" Mwingine atasema; " Tunakokwenda ni kubaya!". Lakini, ni Watanzania wangapi wenye kuuliza maswali haya; " Tumefikaje hapa?" Na " Je, tunaendaje?" Maswali hayo yanamtaka mwanadamu afikiri kwa bidii.
Wakati mwingine nafikiri, kuwa Watanzania tumechoka kufikiri. Hata kwenye maswali magumu yenye kutuhusu tunataka wengine wafikiri kwa niaba yetu. Unaweza kukutana na Mtanzania mwenzako ukamwuliza; " E bwana ee, unafikiri nini juu ya jambo hili?". Jibu lake; " Kwani wewe unaonaje?"- Ni moja ya maswali yenye kuashiria anaykujibu swali lako amechoka kufikiri.
Na wakati mwingine tatizo si kutofautiana kifikra, bali kutofautiana namna au jinsi ya kufikiri. Swali moja, lakini unaweza kuona namna tunavyotofautiana katika kuchagua njia ya kulisogelea ( approach) swali husika.
Na kuna wenye kukimbilia kutafuta njia za mkato. Ndio, majawabu ya mkato. Na baadaye itakuwaje? Inshallah na BwanaYesu Asifiwe!
Maggid Mjengwa,

Iringa
0788 111 765

UJUMBE WANGU:-KUTHUBUTU KUONYESHA MAPENZI/UPENDO NDIYO NGUZO YA MAHUSIANO BORA!!

Kuthubutu kuonyesha upendo wako sio tu maneno mazuri, na sio tu upendo wa matendo au maua na chokleti. Ni kuonyeshana heshima, uaminifu na imani. Pia kuonyesha wepesi wa kuona huruma wakati mwenzako anapokuwa na msongo/matatizo. Kuwa msaidizi mwema na mwenye kusema ukweli.
Kuthubutu kuonyuesha masikitiko yako. Sio kila wakati kujifanya mwenye nguvu(mvumilivu).
Tukumbuke kukaa pamoja  na kupeana mawazo ya maisha..ikibidi kuwa watoto ndani yetu.
Tuwe sisi kwa dadika chache. Dakika chache za furaha., dakika chache za huzuni.Tufanye siku iwe ya sherehe.Tushirikiane katika raha na taabu maishani. Tujipe uaminifu. Tukaribiane na ili kuwa pamoja.

ELIMU :- KISOMO CHA WATU WAZIMA!!!

Elimu haina mwisho hapa akina mama wapo darasani kwa ajili ya kupata ELIMU..angalao kuweza kuandika tu..Inafurahisha kuona walezi wetu wana moyo wa kutaka kupata elimu. Ila nimejiuliza hivi hili darasa ni kwa ajili ya akina mama tu? Maana sioni akina baba hapa.

Monday, September 3, 2012

Taarifa ya Jukwaa la Wahariri Tanzania kuhusu Kuuawa kwa Daudi Mwangosi


TAARIFA YA JUKWAA LA WAHARIRI (TEF) KWA VYOBO VYA HABARI KUHUSU KUUAWA KWA MWANDISHI DAUDI MWANGOSI


UTANGULIZI:

1. Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), limepokea kwa masikitiko makubwa kifo cha mwandishi wahabari wa Kituo cha Televisheni cha Channel Ten, mkoani Iringa, Daudi Mwangosi.

2. Mwangosi ambaye pia alikuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Iringa (IPC), aliuawa akiwa kazini jana, Septemba 2, 2012, wakati polisi walipokuwa wakiwadhibiti wafuasi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

3. Tukio hili linaiingiza Tanzania katika historia mbaya ya ukiukwaji na ukandamizwaji wa uhuru wahabari, kwani ni kwa mara ya kwanza tunashuhudia mwandishi wa habari AKIUAWA WAKATI AKITEKELEZA MAJUKUMU YAKE YA KIHABARI.

4. Taarifa za awali zinaonyesha kuwa Mwangosi kabla ya kufikwa na mauti saa 9.30 alasiri katika kijiji cha Nyololo, Mufindi, alizingirwa na kushambuliwa na polisi waliokuwa katika eneo la tukio. Na hata alipopiga kelele za kuomba msaada, hakusikilizwa na matokeo yake aliuawa na kitu kinachodhaniwa kuwa ni bomu.

5. Kwa kushirikiana na Baraza la Habari Tanzania, TEF tumechukua hatua za haraka za kuunda timu ya uchunguzi wa suala hilo, ambayo itakwenda mkoani Iringa mapema kadri itakavyowezekana, ili kubaini ukweli wa tukio hilo. Lengo la uchunguzi huo ni kuweka kumbukumbu sahihi (documentation) ya tukio hilo la aina yake katika historia ya nchi yetu.

6. Matokeo ya uchunguzi huo pamoja na mwingine unaofanywa na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), ndiyo yatakayotoa mwelekeo wa hatua ambazo TEF inachukua dhidi ya Jeshi la Polisi katika siku chache zijazo.

MTIZAMO NA MSIMAMO WA TEF

Kwa kuzingatia taarifa kutoka Iringa na zile za vyombo vya habari vya jana (Jumapili, Septemba 02, 2012) na leo (Jumatatu, Septemba 03, 2012), TEF ina mtizamo na msimamo kama ifuatavyo:

1. Kwanza tunalaani vikali tukio la kupigwa, kisha kuuwawa kwa mwandishi Daudi Mwangosiambalo limeigusa tasnia ya habari kwamba sasa pengine waandishi wa habari ni malengo “target ya polisi” wanapokuwa kwenye kazi zao.

2. Ieleweke wazi kwamba matukio haya siyo yanaondoa imani ya waandishi wa habari kwa jeshi lapolisi tu, bali yanaweza kuwa chanzo cha uhasama na ufa mkubwa ambao utawanyima wananchi nafasi ya kutumikiwa na pande mbili ambazo zinategemeana.

3. Kwa matukio ya aina hii, tunadhani wakati mwafaka kwa uongozi wa Jeshi la Polisi nchini kuwajibika, kuazia kwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa na uongozi wa Makao Mkuu, akiwamo Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP), Saidi Mwema.

4. Tunasema hivi kwani kuna kila dalili kwamba polisi wanahusika kwa namna moja au nyingine na tukio au/na matukio yaliyosababisha kifo cha Mwangosi, kwani kitendo cha kumzingira tu na kumshambulia kinathibitisha kwamba hawakuwa na nia njema hata kidogo dhidi ya mwandishi huyu.

5. Taarifa ambazo TEF tunazo, pia zinadai kwamba kulikuwa na mpango wa polisi wa “kuwashughulikia waandishi wa habari watatu” (Mwangosi) akiwa mmojawapo na hilo lilionekana likitekelezwa kwa polisi kumshambulia mwandishi huyo, baadaye alipoteza maisha katika mazingira ya kutatanisha.

6. Hili linatiliwa nguvu na tukio jingine la polisi kumpiga na kumjeruhi mwandishi mwingine, Godfrey Mushi ambaye ni mwakilishi wa gazeti la Nipashe mkoani Iringa. Mwandishi wa tatu ambaye hadi tunapoandika taarifa hiyo yumo katika mpango wa ‘kushughulikiwa na polisi’ ni Francis Godwin ambaye ni mwandishi wa habari wa kujitegemea.

7. Vitendo vya aina hii havivumiliki na havipaswi kuachwa kuendelea kwani ni hatari kwa ustawi wa demokrasia na uhuru wa habari nchini. Hatuwezi kuendelea katika mazingira ambayo polisi wanageuka kuwa chombo cha mauaji ya raia badala ya kuwa walinzi wa raia.

8. Kwa maana hiyo, mbali na uchunguzi ambao utafanywa na polisi, tunatoa wito kwa Serikali kuunda chombo huru, ambacho kitabaini ukweli, na matokeo yake yatangazwe kwa umma, huku wahusika wa aibu hiyo wakichukuliwa hatua za kisheria. Tunasema hivyo, tukifahamu kwamba tayari kuna jitihada za kuficha ukweli na kueneza propaganda za uongo kuhusu tukio zima.

9. Mwenendo wa aina hii wa chombo cha dola kuamua kutumia silaha kuua na baadaye kupanga mbinu chafu za kuficha ukweli ni hatari kwa Taifa, na unaiweka demokraisia ya nchi yetu njia panda, huku tukielekea katika hatari ya Taifa kutumbukia katika uovu.
IMETOLEWA NA:
NEVILLE MEENA,
KATIBU MKUU – JUKWAA LA WAHARIRI TANZANIA (TEF)
Source: http://www.wavuti.com

TANZANIA YANGU NA MAKABILA YAKE NA UTAMADUNI WAKE..WAGOGO TOKA DODOMA.!!!

Tanzania ni nchi ambaye ina makabila mengi sana zaidi ya 130..Na kila kabila lina mila na utamaduni wake. Binafsi najivuna sana kuwa mtanzania leo tuwatembelee wenzetu wagogo kwa mtindo wa kuwasikiliza wakiwa wakiimba na kucheza..

JUMATATU NJEMA KWA WOTE....

Sunday, September 2, 2012

HILI NDILO NENO LILILOCHAGULIWA NA BLOG YA MAISHA NA MAFANIKIO KWA JUMAPILI HII YA LEO!!!

Katika maisha yangu  hakuna ZAWADI nilizozipata na ninazozithamini kama vitabu hivi viwili. Maana ni ndivyo vinavyoniongoza katika maisha yangu. Hicho cha kwanza ni MAANDIKO MATAKATIFU YA MUNGU YAITWAYO BIBLIA. Yaani Agano La Kale Na Agano Jipya. Hii nilipata kutoka kwa baba wa nyumba. Na hii ifuatayo ambayo ni HABARI NJEMA KWA WATU WOTE Ambayo ni AGANO JIPYA  kwa KISWAHILI CHA KISASA. Hii nilipewa na baba yangu mzazi . Haya ngoja tuangalie neno la leo:-

Kuna Mungu mmoja na baba wa wote ambaye yuko juu ya wote, afanye kazi katika yote na yupo katika yote. Waefeso 4:6.
JUMAPILI NJEMA KWA WOTE....ANMANI NA UPENDO VITAWALE NDANI YA MIOYO TETU DAIMA.

Saturday, September 1, 2012

MWEZI MPYA:- TUANZE HIVI TUSISAHAU KULA MATUNDA NI MUHIMU KWA MIILI YETU!!

Matunda, tusisahau kula matanda jamani....kwa kawaida inatakiwa tule angalao kila siku matunda kama matano hivi. Lakini kwa bahati mbaya si wengi tuna nafsi ya kula hata tunda moja kwa siku. Na pengine wale wanye nafasi hawali. Jambo hili la kutokula matunda huhatarisha miili yetu kuto jengeka yaani vile virutubisho vya kuujenga mwili na kuuimarisha. kikinga. Na ndio hapo tunapojikuta miili yetu haina kinga za kutosha.
Wote tunajua mwili uwapo dhaifu ni rahisi sana kushambuliwa/kupatwa na maradhi hatari. Kama vile saratani, pia mboga majani nazo husaidia tuzile kwa wingi nazo pia. Kuna wakati unaweza kushangaa, kuona mtu anamaliza mwezi mzima hajala hata tunda moja. Tuchukue ule msimu wa machungwa, unaingia mpaka unaisha hajala hata chungwa moja. Ukija msimu wa maembe nao ni hivyo hivyo. Halafu utakuta maembe yanadondoka tu chini na kuoza na pia wengine wanayaokota na kulisha nguruwe. Au wanyama wengine lakini yeye mwenyewe anajisahau.

Wengi huona ya kwamba matunda siyo sehemu ya vyakula muhimu. Tuache tabia hii tule matunda na tuepukane na maradhi. Ukitaka kulifaidi tunda, basi kula pale ambapo tumbo lipo tupo/kabla hujala kitu chochote tanguliza matunda kwanza na baada ya nusu saa au saa moja, ndiyo unashauriwa ule mlo wako kamili.
NAWATAKIENI JUMAMOSI HII YA KWANZA YA MWEZI HUU WA TISA IWE NJEMA SANA!!!