Monday, May 15, 2017

WANAUME NAO HUNYANYASIKA KIJINSIA MAKAZINI TOFAUTI NA INAVYODHANIWA !

Kama uki google kwa picha ‘Unyanyasaji wa kijinsia makazini’ utashangaa, kwani takribani asilimia 90 ya mapicha picha utakayoyaona yanawaonyesha wanawake wakifanyiwa unyanyasaji wa kijinsia na wanaume.

Lakini ukweli ambao hausemwi ni kwamba wanawake ni wachokozi zaidi ya mara 9 kwa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia katika maeneo ya kazi. Najua kuna baadhi ya wanawake wanaweza kutokwa na povu lakini huo ndiyo ukweli wenyewe.

Kwa kawaida unyanyasaji wa kijinsia ni kitendo cha kumchokonoa mtu wa jinsia tofauti au hata jinsia moja kwa kumfanyia vitendo au ishara za kimapenzi kwa nia ya kumtega, kumshawishi au kumlazimisha kufanya naye mapenzi.

Na hii inaweza kufanywa na mtu mwenye madaraka mahali pa kazi dhidi ya walio chini yake au kati ya wafanyakazi wenyewe kwa wenyewe. Na tatizo hili dhidi ya wanaume limekuwa likikua siku hadi siku katika maeneo ya kazi hapa nchini ni vile tu halisemwi kama linavyosemwa pale muathirika anapokuwa ni wa jinsia ya kike.

Wanawake wamekuwa wakijificha kwenye kichaka cha kujiona kama vile wao ndiyo waathirika wakubwa wa vitendo vya unyanyasaji wa kijinsia mahali pa kazi wakati wanaume kwa upande wao wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya namna hiyo lakini wamebaki wakiumia ndani kwa ndani kwa sababu hawana pa kusemea.

Ni nani asiyejua kwamba wanawake licha ya kuvaa mavazi yenye kuacha sehemu ya miili yao ya faragha wazi lakini pia mikao yao isiyo ya staha inawaweka baadhi ya wanaume katika wakati mgumu na kushindwa kufanya kazi. Hilo linaweza likaonekana si tatizo, lakini je vipi kuhusu mazungumzo yenye kushawishi ngono yanayofanywa na wananawake au vitendo vya kuwashika wanaume sehemu zao za siri ili kupima maumbile yao, vitendo vya aina hii viitweje kama siyo unyanyasaji wa kijinsia. Je vitendo vya kuwatomasa tomasa wanaume kunakofanywa na baadhi ya wanawake pale wanapoelekezwa kazi au kufundishwa kazi fulani huo siyo unyanyasaji wa kijinsia?

Kuna baadhi ya mabosi wanawake wamekuwa wakiwataka kimapenzi wanaume walio chini yao kwa nguvu na kama wakikataa watakiona cha mtema kuni. Wapo baadhi ya vijana wa kiume wamegeuka kuwa watumwa wa ngono wa mabosi wao na hawathubutu kufanya fyoko maana hatma ya kazi yao imo mikononi mwa hao mabosi wanawake.

Kuna haja sasa ya wanaume kusema sasa basi imetosha na sisi tutafute jukwaa la kusemea madhila yetu maana wenzetu wamejiweka kwenye kundi la waathirika wa vitendo hivyo kumbe na wao wamegeuka Chui ndani ya ngozi ya kondoo.

Kwa hisani ya Mtambuzi
JF

No comments: