Monday, September 4, 2017

TUANZE WIKI HII NA NENO FURAHA: HIVI KWANINI KUN SIKU MTU HUKOSA FURAHA?


Ndiyo...Furaha inatokana na ridhiko la ndani la mtu bila kuhusisha vitu vya nje. Mtu akishajua namna sahihi ya kuipata furaha basi hataipoteza kamwe. Yoyote anaeipoteza furaha huyo anakuwa anaitafuta nje yake kwenye mazingira ya nje.....
Lazima atakuja kuikosa siku moja kwasababu mazingura ya nje sio rafiki sana na binadamu kwasababu hubadilika badilika....

Mfano kuna wakati wa jua, masika na kiangazi za kawaida...
Kama umepanga kwenda kulipwa mapato yako fulani na umewekeza furaha yako kwenye hela halafu mvua ikanyesha lazima tu furaha yako itapotea....
Kuridhika kwa ndani kuna maana ya kujikubali jinsi ulivyo bila kutegemea hali ya nje iko namna gani...
Utakapo jikubali namna ulivyo kamwe hutajutia wala kukosa furaha hata siku moja

No comments: