Tuesday, March 13, 2018

UJUMBE WA LEO TOKA KWANGU KUJA KWENU

Mfanyie mtu mambo/jambo mazuri/zuri na mema akiwa hai, kwa sababu chochote utakachomfanyia aliyekufa hakina maana kwa vile hatasikia.
NAWATAKIENI SIKU NJEMA

5 comments:

ray njau said...

Asante sana kwa zawadi njema.
Uwe na siku njema.

Yasinta Ngonyani said...

Kaka Ray ahsante sana. ..hujambo lakin? za masiku jamani....

ray njau said...

Asante sana dadangu.Tashukuru tupo salama kifamilia.Nawatakieni maisha mema kifamilia.

ray njau said...

Wakati mwanaume mumoja anatengeneza motokari, mwengine anamupatia kinywaji cha baridi

MAONI YA BIBLIA
Shukrani

Uchunguzi unaonyesha kwamba kushukuru kuna faida za kimwili, kiakili, na kihisia, kwa hiyo kila mtu anapaswa kuwa mwenye shukrani.
Kushukuru kunaboresha afya jinsi gani?
SAYANSI YA KITIBA INASEMA NINI?

Kulingana na makala ya Harvard Mental Health Letter, “kwa kawaida shukrani inahusianishwa na furaha. Kushukuru huwafanya watu wajihisi vizuri, wafurahie mambo mazuri, huboresha afya, husaidia kukabiliana na hali ngumu, na kuwa na mahusiano mazuri.”
BIBLIA INASEMA NINI?

Biblia inatutia moyo tuwe wenye shukrani. Mtume Paulo, aliyekuwa mwenye shukrani aliandika hivi: “Mjionyeshe kuwa wenye shukrani.” Kwa mfano, ‘alimshukuru Mungu bila kuacha’ kwa sababu watu waliitikia vizuri ujumbe aliohubiri. (Wakolosai 3:15; 1 Wathesalonike 2:13) Furaha ya kudumu haitokani tu na kusema asante kwa ukawaida bali hutokana na kuwa na mtazamo wa shukrani. Mtazamo huo, hutulinda kujiona kuwa na haki fulani, wivu, na kinyongo, tabia zinazoweza kututenga na watu na kufanya tupoteze shangwe.

Muumba wetu ameweka mfano mzuri kwa kuwa mwenye shukrani, hata kwa wanadamu wa hali ya chini! Waebrania 6:10 inasema: “Mungu hakosi kuwa mwadilifu hivi kwamba asahau kazi yenu na upendo mlioonyesha kwa ajili ya jina lake.” Naam, Muumba wetu huona kwamba ni tendo lisilo la uadilifu kukosa shukrani.

“Shangilieni sikuzote. Kuhusiana na kila jambo toeni shukrani.”—1 Wathesalonike 5:16, 18.

Kuwa mwenye shukrani huboreshaje uhusiano wetu na wengine?
MAMBO YALIYOONWA HUONYESHA KWAMBA

Kushukuru kutoka moyoni, iwe ni kwa sababu ya zawadi, maneno ya fadhili, au msaada, hufanya mtoaji ahisi amethaminiwa. Hata watu tusiowajua hufurahi sana tunapowashukuru kutoka moyoni kwa sababu ya tendo la fadhili, kama vile kutufungulia mlango.
BIBLIA INASEMA NINI?

Yesu Kristo alisema, “Muwe na mazoea ya kuwapa watu, na watu watawapa ninyi. Watawamwagia katika mfuko wa nguo zenu kipimo kizuri, kilichoshindiliwa, kilichotikiswa pamoja na kufurika.” (Luka 6:38) Fikiria kisa cha Rose, msichana aliye kiziwi anayeishi katika kisiwa cha Vanuatu, Kusini mwa Pasifiki.

Rose alihudhuria mikutano ya Kikristo ya Mashahidi wa Yehova lakini hakufaidika sana na mikutano hiyo kwa kuwa yeye na hata wengine kutanikoni hawakujua lugha ya ishara. Wenzi wa ndoa wanaojua vizuri lugha ya ishara walipotembelea kutaniko hilo na kuona uhitaji huo, walianzisha darasa la lugha hiyo. Rose alifurahi sana. Alisema hivi: “Ninafurahi kuwa na marafiki wengi wanaonipenda.” Wenzi hao huona kwamba ni baraka kumwona Rose akithamini na kushiriki katika mikutano. Pia, Rose anathamini jitihada ambazo wengine walifanya kwa kujifunza lugha hiyo ili kuwasiliana naye.—Matendo 20:35.

‘Yule anayetoa shukrani zikiwa dhabihu yake ndiye anayemtukuza [Mungu].’—Zaburi 50:23.

Unawezaje kuwa mwenye shukrani?
BIBLIA INASEMA NINI?

Kuna uhusiano kati ya hisia na mawazo yetu. Mwandikaji wa Biblia Daudi alisali hivi kwa Mungu: “Nimetafakari juu ya utendaji wako wote; Kwa kupenda niliendelea kuhangaikia kazi ya mikono yako mwenyewe.” (Zaburi 143:5) Naam, Daudi alishukuru kutoka moyoni. Alichochewa kushukuru kwa sababu ya kutafakari kwa ukawaida njia za Mungu, na alifanya hivyo katika maisha yake yote.—Zaburi 71:5, 17.

Biblia inatoa ushauri huu mzuri: ‘Mambo yoyote yaliyo ya kweli, yaliyo ya kupendeka, yanayosemwa vema, wema wa adili, na jambo lolote la kustahili sifa, endeleeni kuyafikiria mambo hayo.’ (Wafilipi 4:8) Maneno “endeleeni kuyafikiria” yanakazia umuhimu wa kutafakari kwa ukawaida, na kufanya hivyo kutatusaidia kuwa wenye shukrani.

“Moyo wangu utatafakari mambo ya uelewaji.”—Zaburi 49:3.

Yasinta Ngonyani said...

Amina ...ubarikiwe sana kwa neno!